Ilikuwa Jumamosi ya Tarehe 16 Octoba,2010 Kaka DANI na Dada UPENDO walipoamua kuwa mwili mmoja,Harusi iliofungwa pale OVERLAND PARK CHURCH OF CHRIST.
Na baadae kufanywa Adult reception pale CROWNE PLAZA HOTEL.
Kaka Dani akiwa ameshikiria chake wasijempora...kwakweli walipendeza sana!
wageni kibao walikuwepo kushuhudia siku hiyo
maharusi wakisalimia na ndugu na jamaa na jamaa baada ya kuwasili ukumbini
Mama mzaaa chema akitoa nasaha zake ...aiseee mama alinifurahisha sana siku hiyo maana watu walitamani hata aongee usiku kucha!
msione nimependelea mama huyu ila hivi ndivyo ilivyokuwa mara tu mama wa bi harusi mama massawe alipomaliza nasaha zake ghafla wageni waalikwa wote waliinuka kwenye viti vyao na kwenda kumpa hongera kwa shuguli pevu aliofanya mama ..kwakweli ilikuwa safi hiyooo!!!
mtamboni siku hiyo alikuwa mtaalamu wangu SAMCHOM IN DA MIX
Wageni wakipata vinywaji vyao ilimradi kila kiwe safi siku hiyo kwa kweli watu walifurahi smahani hapo camera yangu ilipata kwikwi!
To the left to the right...hivi ndivyo ilivyokuwa ilikuwa furaha ya aina yake kwa kweli
Mkali wa sauti toka kansas city kijana Haule alikuwepo kutumbuiza ebwana jamaa alifunika vibaya mno aliperfom nyimbo kali kwa ajili ya kaka Dani yenye ujumbe mzito ndani yake ebwanaeeh ilikuwa nnooooma hiyo!!
samchom hakuwaacha wageni wakae maana sebene mduara vyote vilikuwepo.....
Obama'z mtoto alikuwepo nae... akiwa amejiachia na kijana Haule hapo
Hapo nikiwa na dada yangu mwenyewe
Motomoto'z wakiwa wamejiachia kwenye kamera ya obama'z mtoto
Kijana haule akiwa amejiachia na na Mtaalamu wa kansas city mwenye Papaa Alex
Kwakweli maharusi walifurahi sana...kwa niaba nzima ya Obama'z mtoto tunawatakia maharusi maisha marefu ya furaha na upendo!!
***********
No comments:
Post a Comment